http://www.ktnkenya.tv\nZimesalia siku kumi na nane pekee kabla ya kung'oa nanga kwa mashindano ya Olympiki. Hata hivyo timu ya Kenya imeamua kuweka vikwazo wakati wa mazoezi kwani hata wanahabari hawataruhusiwa kupiga picha mazoezi yote kama ilivyokuwa hapo awali. Mwanahabari Victor Ogalle anatufungulia jamvi la michezo akituelezea zaidi kuhusu masharti mapya ya timu ya Kenya.